@mwlemiliankatubayemo: Wanauwezo wa kuchafua jina lako ila hawana uwezo wa kuondoa Neema ya Mungu iliyoko juu yako Mke wa Potifa alifanikiwa kuchafua jina la Yusufu Nchi Nzima ila Mungu hakumruhusu mke wa Potifa aiondoe Neema iliyokuwa juu ya Yusufu Neema iliyokuwa juu ya Yusufu ilimwinua tena, ilintambulisha tena, ilimketisha na wakuu tena, ilimpa jina la sifa tena mahali pale pale alipochafuliwa Ninakuombea pamoja na kwamba wamechafua jina lako kama Mungu aliruhusu waone likichafuka, Mungu aruhusu pia waone likisafishwa tena We nyamaza tu kimya nakwambia wataona Neema ya Mungu ikikwinua tena, wataona Neema ya Mungu ikikuketisha na wakuu tena, wamechafua jina lako ila hawajaondoa Neema ya Mungu juu yako Acha Neema ikakuinue na kukutambulisha tena katika jina la Yesu