@realjaymelody: Nilivyokua mtoto nilikua nashangaa sana Kwanini mimi vitu vyangu haviwi kama vya watoto Wengine, nilikosa vingi ambavyo niliamini ni haki yangu kuvipata. Sikujua kama vitu sio rahisi hivyo. Japo wazazi wangu na ndugu zangu walijitahidi sana niishi vizuri kwenye hali yetu ile ile ya umaskini. Ikafika wakati nikajizoesha kwamba kuna vitu sio muhimu kwangu japo watoto wezangu wanavyo. Nikawashawishi mpaka na marafiki zangu kuto kupenda vitu kama Nguo za siku kuu, chipsi,soda 😄 na kadhalika. Asante kubwa kwa wazazi wangu kwa kunilea vizuri na asante pia kwa wazazi wote wanaopambana kwaajili ya watoto wao na familia zao🫡 Now nimekua nimetambua🤔 Bora zamani nilivyokua mtoto