@fertilitybloomtz: 📌 Presha ni nini? Ni hali ya kuwa na shinikizo kubwa au dogo la damu linalopita kwenye mishipa ya damu. ⸻ 🚨 Aina za presha: 1. Presha ya kupanda – damu inapita kwa nguvu kupita kiasi. 2. Presha ya kushuka – damu inapita kwa polepole kupita kiasi. ⸻ ⚠️ Dalili za presha ya kupanda: • Maumivu ya kichwa • Kizunguzungu • Macho kuona ukungu • Mapigo ya moyo kwenda kasi ⸻ ⚠️ Dalili za presha ya kushuka: • Kuchoka sana • Kizunguzungu • Kukohoa au kukosa nguvu • Baridi au ngozi kukosa damu ⸻ ❗ Sababu kuu za presha kupanda: • Chumvi nyingi • Msongo wa mawazo • Kutofanya mazoezi • Uzito kupita kiasi • Kuvuta sigara au pombe ⸻ ✅ Namna ya kujikinga na presha: • Punguza chumvi • Kula matunda na mboga • Fanya mazoezi mara 3 kwa wiki • Kunywa maji ya kutosha • Epuka msongo wa mawazo