@ederaya: KUISHI PAMOJA NA MUME MLEVI. Leo nataka kugusa kwa undani maumivu ya kiakili na kihisia ambayo wanawake wengi hupitia wanapoishi na mume mlevi... Wakati tunapozungumza kuhusu ndoa, mara nyingi tunafikiria furaha, mshikamano na maelewano.... Lakini kwa wengine, ndoa imekuwa chanzo cha maumivu makali, hasa pale ambapo mmoja wa wenza anajitumbukiza kwenye ulevi.. Mke anapokuwa na mume mlevi, mara nyingi maisha yake hubadilika kutoka kwenye furaha ya ndoto za ndoa hadi mateso ya kimya... Anapoona mume akirudi usiku akiwa mlevi, moyo wake unadunda kwa hofu: “Leo itakuwaje? Je, atakuwa na hasira, matusi au ukatili?” Saikolojia ya familia inafafanua hali hii kama emotional burnout — kuchoka kabisa kiakili na kihisia kwa sababu ya mzigo wa ndoa.... Watoto wanaoshuhudia baba mlevi huathirika kwa kiwango kikubwa..... Mara nyingi hupata; Matatizo ya kujiamini, Kushindwa kujifunza vizuri shuleni, Wengine hujiingiza katika urafiki mbaya hata wakijaribu kujifunza jinsi mzazi wao alivyo mlevi... Hii ndio maana EDERAYA tunasema; Ulevi sio tatizo la mtu mmoja ni janga la Familia... Wanasayansi wa afya ya akili wanasema..... Mwanamke anayeishi na mwanaume mlevi hupata msongo wa mawazo wa muda mrefu, ambao hupelekea hatari ya shinikizo la damu, Magonjwa ya moyo, Kuumwa Mara kwa mara kwa sababu ya kushuka kwa kinga ya mwili... Biblia na maandiko ya kiroho hutufundisha kwamba ndoa ni agano la amani na heshima. Lakini ulevi huleta giza katika agano hilo.... Hitimisho...... Ndugu zangu, mateso ya kuishi na mume mlevi si jambo dogo. Ni hali inayochosha akili, moyo na mwili. Lakini kumbuka: wewe si mnyonge, wewe ni shujaa. Kuna msaada wa kisaikolojia, Usinyamaze tafuta msaada kwa Mwanasaikolojia. Naamini kwa msaada huu, kila mmoja anaweza kupata nguvu ya kusimama, kujilinda, na hata kumsaidia mwenza wake pale inapowezekana... Familia yenye mzigo wa ulevi inahitaji tiba, si lawama pekee.. Zingatia: ..... MKE: Hata ukiishi katika nyumba yenye giza la pombe, unaweza kuwa taa inayong'aa kwa imani na uvumilivu. Maombi yako ni mbegu ya mabadiliko ya mume wako, hata kama majibu yanachelewa. Siku moja yatachipua kwa wakati wa MUNGU. MUME: MUNGU anakupenda hata kama upo kwenye giza la ulevi, Ulevi wako si mwisho wa maisha yako. Kila hatua unayoichukua kuacha ulevi ni ushindi wako wa Kiroho. MUNGU haachi wanaoanguka. See You Above. EDERAYA-- Sauti ya Faraja na Matumaini. Mwanasaikolojia na Mshauri Nasaha. [email protected]. Kwa huduma ya msaada wa kisaikolojia, pamoja na semina kuhusu afya ya Akili. Mawasiliano. Simu: 0674400743 WhatsApp: 0748900743