@veriafya: Vitamin A huboresha hali ya afya ya mfumo mzima wa Njia ya Hewa na huzuia kupata Nimonia (Pneumonia) ndio maana watoto wakifika Miezi Sita lazima wapate Vitamin A na kuanzia hapo kila Miezi 6 hupewa Dozi ya Vitamin A kwasababu ukosefu wake unachangia katika kudhoofisha mfumo mzima wa Njia ya Hewa Vitamin A hupatikana kwa wingi kwenye Mboga za Majani kama Mchicha, Spinachi na Brokoli, na Matunda kama Embe, Tikitimaji, Zabibu na Papai, na Viungo kama Nyanya, Pilipili hoho, Karoti pamoja na Maboga. Prof. Karim Manji Mhadhiri - Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Video: Elimu ya Afya Online TV