@ahmadrubibi: Taarifa zinaeleza kuwa boti hiyo ilikumbwa na upepo mkali na mawimbi makubwa wakati ikisafiri kutoka Kigoma, Tanzania kuelekea Baraka, nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Kutokana na hali mbaya ya hewa katika Ziwa Tanganyika, boti ilianza kuyumba na kuwa katika hatari ya kuzama. Ili kupunguza uzito na kujaribu kuinusuru, wahudumu na wasafiri walilazimika kutupa baadhi ya mizigo ya biashara majini ili boti ipate nafuu na kurejea katika mlinganyo. Tukio hilo liliripotiwa kutokea katika ukanda wa maji ya Burundi ndani ya Ziwa Tanganyika mnamo January 8, 2026. Reporter: Bandidu Mbwa Koko #tanzaniatiktok #kenyatiktok #burunditiktok🇧🇮 #congokinshasa243🇨🇩 #fyp