@ufr_tz: Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora linamshikilia Kange Thabiti (45), mkazi wa Kiloleni mkoani Tabora, kwa tuhuma za kujaribu kufanya utapeli kwa baadhi ya viongozi wa mkoa huo kwa njia ya simu. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo machi 16, 2026 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha amesema mtuhumiwa huyo alijaribu kumtapeli kwa kujitambulisha kuwa yeye ni Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa, akidai anahitaji mchango kwa ajili ya harusi ya binti yake. RC Chacha ameeleza kuwa baada ya kupokea ujumbe huo aliamua kuwasiliana moja kwa moja na Waziri Mchengerwa ili kuthibitisha taarifa hizo. Baada ya kufanya mawasiliano, Waziri Mchengerwa alikanusha kuhusika na ujumbe huo na kuagiza mtuhumiwa huyo atafutwe na kukamatwa mara moja. Aidha, Chacha amesema mtuhumiwa huyo amekuwa akitumia laini zaidi ya moja za simu kufanya jaribio la utapeli kwa viongozi mbalimbali mkoani Tabora. Kwa mujibu wa RC Chacha, mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho Machi 17, 2026, kujibu tuhuma zinazomkabili. 📻 Sikiliza Uyui FM Radio popote ulipo duniani, bofya kiungo (link) kwenye bio yetu. #2026Fanikisha #tunasambazaunyamwezi #Fanikisha #radioyetusautiyetu
Uyui FM Radio
Region: TZ
Monday 16 March 2026 16:16:37 GMT
Music
Download
Comments
Dory Kapinga :
huzuni baba wa watu alikuwa anatafuta rizki mwee maisha haya 😭😭
2026-03-16 19:40:56
461
liwa :
😅watu sio waoga jamani khaaa💔🙌
2026-03-16 17:55:26
834
Mbunge wa TikTok 🇹🇿 :
huyu mkuu wa mkoa yupo smart sana, very very obligater 🥰🥰🥰🥰🙏🙏🙏
2026-03-16 19:11:17
313
mdogo mooh=🔞 :
kama una miaka 20 adi 35 hauna nyumba ,hauna gari,hauna kiwanja na hauna pesa benk bas usijaly tupo wengi kama wew..!🥺
2026-03-16 21:15:27
176
fizoboy :
hongera sana mkuu wa tabora tokomeza vibaka na matapeli
2026-03-16 17:48:01
226
Suleiman :
amefanana sana na Depu
2026-03-16 18:18:22
136
_BALOZ_XXIII🇹🇿 :
kumbe MILIONI 10 ni kama chai kwao
2026-03-16 20:51:52
109
charity kidoa :
baba aibu gani hii jaman 🥺🥺
2026-03-16 18:13:52
119
magreth♥️lucas🎀🎀 :
mmmmmmh mbon ni mtu mzima sana mpka aibu MUNGU wangu Eeeee 🥺🥺
2026-03-16 18:03:57
150
winniekidot :
Aibu naona miye🙌🏻
2026-03-16 19:17:21
101
𝐍𝐆 𝐍𝐢𝐜𝐡𝐨𝐥𝐚𝐮𝐬²³ :
Ila Tabora c ndo makao makuu ya Wizi Tanzania 😃 Pambana Mkuu Mji uwe msafi🙏
2026-03-16 17:51:39
87
mr karim💪 :
😳😳mjombaa jamn
2026-03-16 19:31:39
29
user6324814206170 :
hongera mkuu wa tabora tunataka watumishi kama wewe Asante sana
2026-03-16 17:37:49
113
Khadija Massawe :
jamani baba mtu mzima jamani mungu wangu
2026-03-16 18:05:44
87
🌸Kidoa_tz✨🦋 :
Naombeni mnifollow vipenzi vyangu nawapenda❤️
2026-03-16 19:43:02
15
josure 39 :
njaaa mbaya sana
2026-03-16 17:38:30
50
Mumy Chaya🥰 :
ni maisha tu 🥺 Allah atuhifathie baba zetu ni kuhangaika kwajili ya familia
2026-03-17 09:46:28
16
MA ❤️ MKUBWA. :
dah!mbaba kabisa,ila njaa hizi🙌🙌🙌
2026-03-16 18:59:43
30
SIMBA FASHION :
mweshimiwa wapo wengi sana nawapongeza vijana wako wako vizuli sana
2026-03-16 19:22:59
51
ben kapi :
miaka 45 hapana, labda kuanzia 55 sawa
2026-03-16 17:48:47
74
jesta6 :
mtume
2026-03-16 17:36:39
30
SIDE ALEX :
Bado Chief godlove
2026-03-16 18:42:27
52
Alexander..19 :
kazi nzuri makamanda...safi sana
2026-03-16 18:45:14
16
lyne Doran🌹 :
mweee danga langu jaman ilikuwa ela ya kodi😂😂
2026-03-17 06:11:04
11
kioo changu🥰🌹 :
hongera sana mh.mkuu wa mkoa kwa kukamata tapeli wanatusumbua sana hawa
2026-03-16 21:09:11
10
To see more videos from user @ufr_tz, please go to the Tikwm
homepage.