@afya_pointmart: Twende kutazama faida nyingi za bamia. . Kudhibiti Sukari Mwilini Hii ndiyo faida maarufu zaidi. Bamia ina vimelea vinavyosaidia kupunguza ufyonzwaji wa sukari kwenye utumbo, hivyo kusaidia watu wenye kisukari (Type 2) kuwa na kiwango imara cha sukari. 2. Huboresha Mfumo wa Meng'enyo Ule uteute wa bamia unasaidia "kulainisha" utumbo. Inasaidia sana kuzuia choo kigumu (constipation) na kufanya upatikanaji wa choo uwe wa haraka na bila maumivu. 3. Kupunguza Uzito Maji ya bamia yana kalori chache sana lakini yanakufanya ujisikie umeshiba kwa muda mrefu. Hii inazuia hamu ya kula ovyo asubuhi, jambo linalosaidia kupunguza uzito kwa njia ya asili. 4. Kuimarisha Kinga ya Mwili Bamia ina kiasi kikubwa cha Vitamin C na viini-lishe vya kuzuia sumu (antioxidants). Kunywa maji haya husaidia mwili kupambana na magonjwa madogo madogo kama mafua na kikohozi. 5. Afya ya Moyo na Kupunguza Kolestrol Ule ute wa bamia unasaidia kunasa kolestrol mbaya wakati wa mmeng'enyo na kuiondoa mwilini badala ya kuifyonza kwenye damu. Hii inalinda mishipa ya moyo isiwe na mafuta. 6. Afya ya Ngozi na Nywele Vitamin A na C zilizomo husaidia ngozi kuwa na unyevu (glow) na kuzuia mikunjo. Pia, husaidia kuimarisha mizizi ya nywele na kuzifanya ziwe na mng'ao. 7. Kuimarisha Mifupa Bamia ina Vitamin K na madini ya Folate ambayo ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha mifupa na kuzuia magonjwa ya mifupa kama osteoporosis.#flypシ#afya #viralvideo #usa🇺🇸 #kenyantiktok🇰🇪