@habarimpya_tv: Katibu Tawala wa Wilaya ya Arusha, Dkt. Jacob Julius Rombo, ametoa onyo kali kwa watu wote wanaomiliki na kuendesha gereji bubu zinazofunga na kuuza vifaa haramu vya pikipiki, akisisitiza kuwa operesheni inayoendelea haitawalenga waendesha bodaboda pekee bali itawafikia pia wahusika wote wa mtandao huo. Amesema kuwa baadhi ya gereji hizo zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa kuenea kwa matumizi ya taa zisizoruhusiwa na 'trampa', hali inayohatarisha usalama na kuchochea vitendo vya uhalifu. Hivyo, yeyote anayejihusisha na biashara hiyo anatakiwa kusitisha mara moja kabla hatua kali za kisheria hazijachukuliwa dhidi yake. Dkt. Rombo amesisitiza kuwa Wilaya ya Arusha kwa sasa inapokea wageni wengi na inaendelea na maandalizi ya ujio wa wageni wakubwa, hivyo haiwezekani kuruhusu vitendo vinavyoweza kuchafua taswira ya jiji au kuhatarisha usalama wa wananchi na wageni hao. Aidha, ametoa wito kwa wote wanaojihusisha na biashara hizo haramu kuacha mara moja, akionya kuwa watakaobainika watachukuliwa hatua kali bila huruma. Ameongeza kuwa lengo la operesheni hiyo ni kuhakikisha utulivu, usalama na nidhamu vinatawala katika jiji la Arusha.
HabarimpyaTv
Region: TZ
Friday 27 March 2026 06:04:43 GMT
Music
Download
Comments
abdylugete :
hii inchi ni ya ki maku sana
2026-03-27 07:17:18
252
Michael mshiu :
mkuu ni sawa ila mkuu na wanaotengeneza
2026-03-27 07:19:22
67
Time and Time again :
Safi sana 👏👏👏,hizi kitu zinasababisha ajali kila siku.Viongozi wa Arusha wanafanya kazi nzuri.
2026-03-27 06:43:09
20
Warushegang :
hii nchi ya ovyo sana ya hovyo sana
2026-03-27 09:52:38
31
bobolito :
who is a importer who charges import duties?
2026-03-27 14:00:49
8
Eddy Chulbul Shibulb :
2026-03-27 15:29:54
18
lang'ata 🛣️ :
mungu atupe magari tu maan izi dharau zimezidi
2026-03-27 18:55:39
10
verena :
Kazi nzuri M barikiwe sana Bora muwakamate na taa zitolewe
2026-03-27 13:07:47
4
🚛little driver 🚛 :
hii nayo nizaidi ya utarihi sema amjui2
2026-03-27 08:26:45
19
#DMS :
Iyo imekaa sawa sana mikelele jau
2026-03-27 09:03:15
6
Charles :
kamata wanao tengeneza kwanza!?
2026-03-27 17:12:09
18
J%seph Felician :
safi sana.yanaumiza macho
2026-03-27 14:10:45
1
Abuu Madina :
2026-03-29 11:22:32
2
King Kiaratu🫅🫅 :
swali.zimeingiaje dukani?
2026-03-28 11:14:14
6
Lulu.cheche.chech :
Asante Yesu jamani bodaboda kelele nyi gi sana
2026-03-27 10:51:29
5
Bariki Naftali :
Safiii sanaaa mkuuu
2026-03-27 08:52:26
8
TOTO TUNDU NJOMBE HOM :
erim mmmm
2026-03-30 20:46:09
1
jet mpemba :
akili ndogo sana
2026-03-28 16:57:44
3
Frank Makweta :
safi officer 👍👍👍
2026-03-28 01:47:18
2
fundi homa :
hiyo haiko sw
2026-03-29 20:59:47
1
innossa :
2026-03-27 17:05:23
4
Malick abby :
Safiiii
2026-03-27 14:33:15
2
Jose G :
asante
2026-03-27 09:46:11
2
dady official🇹🇿 :
hii ich ishkua yakiwaki🥺🥺
2026-03-29 00:56:52
1
wakiristo famiry :
hii Tanzania inaenda wapi jamani
2026-03-28 12:29:08
3
To see more videos from user @habarimpya_tv, please go to the Tikwm
homepage.