@asam.media.group: *SIMAI AISHAURI SERIKALI ZAN ID ITUMIKE KUSAJILIA LAINI ZA SIMU* Mbunge wa Bunge ka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Baraza la Wawakilishi Zanzibar ambae ni Mwaakilisji Jimbo la Tunguu, Simai Mohamed Said, ameishauri Serikali kuruhusu matumizi ya Kitambulisho cha Mzanzibar Mkaazi katika usajili wa laini za simu ili kupunguza usumbufu kwa wananchi ambao bado hawajapata kitambulisho cha NIDA. Akichangia mjadala wa bajeti ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Tanzania katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa Bunge la 13, Mkutano wa Tatu, Kikao cha 20 kilichofanyika Dodoma, Simai amesema kuwa wananchi wengi hasa Zanzibar wanapata changamoto kubwa kusajili laini kutokana na kukosa vitambulisho vya NIDA ambavyo kwa sasa vinahitajika kisheria. Amesema kuruhusu matumizi ya Kitambulisho cha Mzanzibar Mkaazi kutasaidia kuondoa adha hiyo na kuwezesha wananchi wengi zaidi kupata huduma za mawasiliano bila vikwazo visivyo vya lazima. Katika mchango wake, Mbunge huyo pia ameitaka Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu mgawanyo wa mapato yatokanayo na sekta ya mawasiliano, akitaka kuelezwa wazi namna Zanzibar inavyonufaika na mapato hayo ndani kupitia Mitandao ya simu. Amehitimisha kwa kusisitiza kuwa maboresho katika sera na mifumo ya mawasiliano yataongeza upatikanaji wa huduma kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi, hususan katika maeneo ya visiwa vya Zanzibar.
Asam Media Group
Region: TZ
Friday 01 May 2026 11:41:33 GMT
Music
Download
Comments
Ochu :
Hongera kiongozi hapa umeongea point
2026-05-01 12:41:38
49
creative Jr :
Poyoyo hili
2026-06-11 02:19:58
1
feso :
allah akulinde
2026-06-11 19:32:48
1
fire :
umeongea point kweli
2026-06-09 17:21:52
0
Viewjustcode :
Nida sio mambo ya muungano
2026-06-10 06:16:19
2
Abdulmalik Haji :
Hongera Mh: Simai kwa maslahi ya Zanzibar
2026-05-01 14:47:52
22
Haroun Suleiman :
nida ndo nini
2026-06-10 15:38:16
1
shibuy :
upo sahihi sanaaaa🥰
2026-06-10 22:32:42
1
Mariam & Mbwana :
nakupenda baba ang
2026-06-10 11:33:19
3
Mr Mani :
ume ogeya jambo 1 zuri sn
2026-05-01 19:28:05
7
harus mkt :
saluti kwako umeongea point
2026-06-11 11:14:55
1
@tumayra saleh :
mh simai yupo mbele ya muda allah bless u
2026-05-22 06:28:32
3
haynuu :
kweliii
2026-05-01 12:27:24
9
bnmuslim :
kweli kabisa mh smayi
2026-05-03 08:23:57
2
Mwihindiwetu :
Hamna hata kofi 😅 Haya ☺️
2026-05-02 11:43:54
2
Prince Asheil :
kabisa ankal
2026-05-01 19:29:42
2
mula said mula :
kweli
2026-05-01 19:47:36
2
Shuu@12345 :
Fact🥰🥰🥰🥰🥰
2026-05-01 14:20:52
2
lamha💋💋💋 :
sawa sawa mkuu umeongea
2026-05-01 18:44:39
2
MANNAL :
Asntt
2026-05-01 19:34:14
1
user79051109709373 :
Kwani uumbe zanzibar wakati c mzanzbar
2026-05-01 14:45:55
2
sarah juma :
kweli kabisa
2026-05-01 13:44:54
1
Fedrick giyam :
sahihi sana
2026-06-11 17:36:38
0
Mamu Morogoro :
SAHIHI MH SIMAI
2026-06-11 18:49:26
0
ruqaiyah uturuki :
good
2026-05-01 13:12:05
0
To see more videos from user @asam.media.group, please go to the Tikwm
homepage.