@officialmzumbeuniversity: Jamii ya Chuo Kikuu Mzumbe wakisindikiza miili ya marehemu Bi. Witness Samora Samila (Mwanafunzi wa mwaka wa pili aliyekuwa akisoma Shahada ya Awali ya Uhasibu na Fedha katika Sekta za Umma) na Bi. Nyabatende B. Julias (Mwanafunzi wa mwaka wa tatu aliyekuwa akisoma Shahada ya Awali ya Usimamizi wa Rasilimali Watu) ikiondoka katika Ukumbi wa Samora, Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi Kuu Morogoro baada ya ibada ya kuaga iliyofanyika tarehe 08 Mei 2026. Hali ya huzuni na simanzi ilitawala miongoni mwa wanafunzi, watumishi pamoja na ndugu wa marehemu hao waliokusanyika kutoa heshima za mwisho kwa wapendwa wao.