@streetjournalisti: ⚠️ (NI UZITO WA TANI 150 NA SIO UZITO WA MITA 150 🙏) Huyu ndiye mnyama mkubwa zaidi duniani, lakini cha kushangaza si ukubwa wake pekee bali namna anavyomlea mtoto wake chini ya maji. Mama nyangumi humnyonyesha mwanae kwa “kupuliza” maziwa yenye mafuta mengi moja kwa moja mdomoni kwa sababu haiwezekani kunyonya kawaida baharini Kama ilivyo kwa Binadamu. Maziwa hayo huwa ni mazito kama Cream/Dawa ya Meno ili yasichanganyike haraka na maji ya bahari, na humsaidia mtoto kuongeza zaidi ya kilo 50 kwa siku. Licha ya uzito wake mkubwa unaofikia zaidi ya tani 150, nyangumi huishi kwa kula viumbe wadogo sana baharini na huwasiliana kwa sauti zinazoweza kusikika mamia ya kilomita chini ya maji. 🌊🔥 #StreetFacts #inashangaza