@chawamata_tv: VIDEO: Mbunge wa Jimbo la Mlalo kupitia chama cha CCM, Rashidi Shangazi amesema pamoja na Jeshi la Polisi kuboresha eneo zima la usalama barabarani, ni lazima kutambua kwamba madereva walio wengi hawana mikataba ya kazi. Akizungumza Bungeni leo wakati wa kuchangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, amesema madereva wengi wanategemea jasho la kila siku ndipo maisha yao yaende. Amesema kwa madereva wanaofanya mchakato wa kuhuisha leseni baada ya muda wake kuisha, kumekuwa na ucheleweshaji wa zaidi ya mwezi mmoja kupata mafunzo hayo jambo ambalo linawasumbua sana. Aidha, Shangazi amesema mafunzo hayo ni muhimu sana lakini ni bora nguvu kubwa zaidi ikawekwa kwa wale wapya wanaotafuta kuingia kwenye kazi hiyo ya udereva. Ametumia nafasi hiyo pia kuliasa Jeshi la Polisi kukaa pamoja na wadau wa vyombo vya moto kupitia vyama vyao kama TATOA, TAMSTOA na TABOA, akisisitiza umuhimu wa waajiri kuwa na mikataba rasmi na madereva. Amesema kitendo cha dereva kufanya kazi bila mkataba ni hatari sana, kwani wapo wanaosafirisha mizigo yenye thamani kubwa lakini wanaweza kupigiwa simu na mwajiri na kuambiwa waache gari njiani huku mtu mwingine akipelekwa kulichukua. Shangazi ameitaja sekta ya udereva kuwa ni moja ya sekta zilizoajiri watu wengi sana na kama ajira hizo zingekuwa rasmi, Serikali ingeweza kupata mapato zaidi kupitia kodi. Akimalizia, amegusia suala la mafao kwa madereva baada ya kustaafu, akisisitiza wawekwe kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii ili nao waweze kuishi kama wafanyakazi wa sekta nyingine. Shangazi ameendelea kuonyesha mchango wa dhati katika sekta ya udereva akiwa na kiu pamoja na shauku kubwa ya kutaka kuwasaidia madereva wa Tanzania. #ChawamataTV #10KFollowers #Asanteni #DarEsSalaam #Tanzania #Bongo #Habari #HabariLeo #BreakingNewsTZ #TanzaniaNews #BongoUpdates #TzUpdates #TzNews #BongoMedia #MediaTanzania #OnlineTV #TrendingTZ #TanzaniaTrending #ViralTZ #TeamChawamata #SupportLocal #MadeInTanzania #RoadTo100K #instagramtanzania
CHAWAMATA TV
Region: TZ
Monday 25 May 2026 10:19:57 GMT
Music
Download
Comments
Sure_boy26 :
Mtu wa maana kabisa huyu
2026-05-25 14:06:43
61
NGOSHA 🔥🔥TZ 🇹🇿🔥🔥 :
mambo yameanza kunoga Sasa 🤲
2026-05-25 11:09:21
37
360 :
mungu akupe afya mzee
2026-05-25 15:31:45
18
feisaly :
mungu akuweke sana ww
2026-05-25 10:29:32
13
Legend… :
Hongera sana mh mbunge.
2026-05-25 17:12:00
6
Idd Mahaba 💗 :
Ahsante 🎙️studio Mambo yanaanz kunoga ss
2026-06-16 15:37:57
3
Moshi dotto :
Asnte sana Baba yetu kakuliona hilo Mungu akupe maisha marefu sana 🙏
2026-06-17 02:33:54
3
Bahati Sunzu paulo :
safi sana 100000%
2026-05-25 15:27:15
6
DARALI MUWAMINIFU BAGAMOYO :
mtu wa nguvu xana uyu baba Asante baba🥰🥰🥰🥰
2026-05-27 08:05:59
8
Brayvan :
Mambo ndio haya Sasa
2026-06-08 15:40:35
0
A :
kweli mkuu
2026-05-25 12:08:57
4
raphael :
asante sana utusemee
2026-05-25 19:18:23
1
Faustine Magobe :
mungu akulide san huko uliko
2026-06-23 07:06:19
1
Emmanuel Igendezi :
nimependa hiiyo wewe ni mtu wa nguvu sana
2026-05-30 17:38:31
2
Jose Paroko :
Barikiweee
2026-05-25 11:29:46
4
EKH628🇹🇿🇹🇿 :
Mia tena
2026-05-25 15:29:02
2
FREDY BOY💙❤💙TZ :
Rispect
2026-05-25 19:18:15
1
Moshi dotto :
Saf sana Mheshimiwa mwenyezi mungu akupe afya njema kwa kutupambania Ma dereva🙏
2026-05-25 15:16:47
8
prezzy Dar :
respect
2026-05-25 11:56:05
5
wamlevimasaka :
Asante kaka agiza jambo power
2026-05-25 17:30:49
3
KANGEMI BRYTONIC :
msemaji wetu sasa ndiyo huyu mwamba, mtu wa maana sana
2026-05-26 05:47:48
4
Muddy Omary :
mambo nimoto ss
2026-05-25 11:12:30
4
Charles Mmbaga :
Mh.unatupambania sana Mungu akulinde ktk majukumu yako
2026-05-28 14:19:37
3
@Wizzo😎💪 :
nakubali mbunge🫡
2026-06-04 16:13:27
1
Chelu Boy :
Mungu akupe hitaji la moyo wako
2026-05-25 16:55:29
1
To see more videos from user @chawamata_tv, please go to the Tikwm
homepage.