@abdulazizielajemi: ✨ SWALA YA TOBA NA JINSI YA KUSWALI ⬇️⬇️ 1_UDHU☘️ chukua udhu kwa usahihi kwani Mtume (s.a.w) anasema "Atakae tawadha Kisha akaswali rakaa mbili Allah humsamehe madhambi yake". 2_NIA☘️ Siku zote Nia ipo moyoni mwako, tia Nia unaswali rakaa mbili za kutubia kwa Allah kwa makosa uliyofanya. 3_SWALI RAKAA 2☘️ Rakaa ya kwanza utasoma suratul Faatiha na sura yoyote unayoiweza, Kisha rakaa ya pili hivyo hivyo. 4_ISTIGHFARI☘️ Baada ya Salam usiinuke Baki hapo hapo, keti kwa unyenyekevu, Lete istighfari kwa wingi. 🤲Omba msamaha kwa dhati mbele ya Allah,mlilie akusamehe madhambi uliyoyafanya. ✨ MASHARTI YA TOBA ⬇️⬇️ ☘️Kujutia moyoni madhambi uliyofanya. ☘️Kuacha papo hapo dhambi hiyo uliyofanya ☘️Kuweka azma ya kutorudia tena dhambi hiyo ☘️Kuomba msamaha kama ulimkosea mtu au kurudisha haki yake. NB:Swala hii utaswali muda wowote isipokuwa nyakati ambazo ni makruhu au haramu kuswali. mfano Wakati jua linachomoza au linapozama ✨ والله أعلم ✨ #islamicvideo#eidmubarak #toba #fyp #viral ☘️ Usisahau KUFOLLOW page hii@guide_qalam ili uendelee kujifunza uislamu wako kupitia mawaidha, nasaha, Qur'an na maneno ya busara.