@health_farm_tz: Baada ya hedhi kukoma (menopause) kiwango cha hormone muhimu ya estrogen hushuka kwa kasi hali ambayo huleta mabadiliko ya ghafla katika mwili wa mwanamke. Moja kati ya athari muhimu zaidi ni mabadiliko katika ujazo (density) wa mifupa ya mwanamke, kupungua kwa kiwango cha hormone ya estrogen husababisha mifupa kuwa dhaifu na laini hali hii kitaalamu inajulikana kama Osteoporosis. Halii hii huongeza hatari ya kuvunjika kwa mifupa kwa urahisi mno isivyo kawaida, na ndio maana wanawake wengi umri wa kukoma hedhi au waliokwisha koma hedhi hukabiliwa na changamoto za mifupa. Kuna njia kadhaa za kupunguza hatari hii ya kuvunjika kwa mifupa na moja wapo ni matumizi ya virutubisho muhimu vya madini ya calcium na vitamin D ambavyo husaidia kujenga mifupa na kupunguza kasi ya mifupa kudhoofika kama alivyoeleza Dr Ngarina. N.B Kwenye Video ni Dr Matilda Ngarina, Bingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi na mkuu wa kitengo cha uzazi pandikizi kutoka Hospital ya Taifa Muhimbili (MNH) akizungumza kuhusu athari na dalili za Hedhi kukoma (menopause) katika tukio liloandaliwa na BarbaraHassan foundation. ELIMIKA, HAMASIKA, CHUKUA HATUA KABLA MWILI HAUJACHOKA! Credit: @barbarahassanm @simulizinasauti #healthfarmtz #menopause #menopausesupport #tiktokviral #tanzaniatiktok