@veriafya: Umewahi kusikia nini kuhusu uhusiano wa Mwanaume kufanya Punyeto na kupungua kwa Nguvu za Kiume? Kwa mujibu wa Dkt. Sadru Mohamed, Mwanzilishi wa App ya AfyaChap na Mkurugenzi wa Kliniki ya Madaktari Bingwa ya Msua Polyclinic iliyopo Musoma, Mkoa wa Mara, upungufu huu hautokani na kitendo chenyewe, bali hutokana na Ubongo kuzoea mazingira yasiyo ya uhalisia mfano Video au picha za ngono na mgandamizo wa mkono, jambo linalomfanya mtu ashindwe kufurahia au kushiriki kikamilifu tendo la kawaida la ndoa na mwenza wake. Mahojiano haya yamefanyika kupitia kituo cha Bongo FM.