@official_tpdf: Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salum Haji Othman ameweka jiwe la Msingi katika Ujenzi wa Kijiji cha burudani kilichopo katika Kambi ya Jeshi Kisarawe Mkoani Pwani leo tarehe 08 Juni 26. Akizungumza na Maafisa na Askari wa Kikosi cha mawasiliano Kisarawe, Luteni Jenerali Othman amesema kuanzishwa kwa miradi hii kutasaidia kikosi kutatua changamoto za mbalimbalii. Miradi iliyoanzishwa ni pamoja na Ujenzi wa uwanja wa michezo, maegesho ya magari ya mizigo, Ujenzi wa Ukumbi wa Burudani na Ujenzi wa kituo cha mafuta. Aidha, Luteni Jenerali Othman amewataka wanakikosi kuepuka tabia zisizofaa ikiwemo matumizi ya madawa ya kulevya, matumizi mabaya ya mitandao ya Kijamii, uraibu wa kushiriki michezo ya kubashiri na ulevi uliokithiri. Pia, wanakikosi wametakiwa kuyaishi maneno manne kwa mwanajeshi ikiwemo nidhamu nzuri, Utii, Uhodari na Uaminifu, maneno ambayo hayana budi kuzingatiwa wakati wote. Naye, Kamanda Kikosi cha mawasiliano Kisarawe Kanali Mwakisamba amemshukuru Mnadhimu Mkuu Luteni Jenerali Salum Haji Othman kwa kuweka jiwe la msingi kujengwa kwa miradi ya kikosi, na kuahidi kukamilisha miradi hiyo. Hafla hiyo ilihudhuriwa na maafisa Jenerali na Wakuu wa Vikosi kutoka Kanda ya Pwani na Dar es Salaam pamoja na Wanakikosi.

LIEUTENANT 🫡
LIEUTENANT 🫡
Open In TikTok:
Region: TZ
Tuesday 09 June 2026 20:26:36 GMT
3987
188
2
1

Music

Download

Comments

intovert40
🤐 :
one day nitaitumikia nchi yangu🙏 tanzania
2026-06-10 06:48:49
0
malume7843
peace dady 🪖🌍 :
🇹🇿🇹🇿🪖💪
2026-06-09 22:21:42
0
To see more videos from user @official_tpdf, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos


About