@health_farm_tz: Katika mahojianao yaliyofanywa na #Mwananchidigital na Daktari bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake na mkuu wa kitengo cha uzazi pandikizi kutoka hospitali ya taifa Muhimbili (MNH) Dr Matlida Ngarina anaeleza kuwa:- wakati wa mchakato wa uzazi pandikizi (IVF) Kuna baadhi ya wanawake hukabiliwa na ukosefu wa mayai licha ya kuchomwa sindano za dawa ya kuchochea uchavushaji wa Mayai. Ametaja pia kuna baadhi ya wanawake wanaweza kutoa mayai na kufanikiwa kurutubishwa na mbegu za baba lakini vijusi vinavyozaliwa hapo vinakuwa havina ubora stahiki wa kutengeza kiumbe kamili. Hii imekuwa ni moja ya changamoto kubwa inayowakabili wanawake wengi sana wanaotazamia kufanya IVF kama njia pekee iliyobaki kwa ajili ya kutimiza ndoto ya kuitwa mama au baba. Kwa Mujibu wa Dr Ngarina, amesema unaweza kupata Mayai na kurutubisha vizuri lakini vijusi visiwe na ubora, Na cha msingi ni kwamba swala la kupata mtoto linategea zaidi pande zote mbili baba na mama hivyo afya ya uzazi ni muhimu kwa jinsia zote mbili. ELIMIKA, HAMASIKA, CHUKUA HATUA KABLA MWILI HAUJACHOKA! CREDIT: Full Video Ipo YouTube @mwananchidigital #healthfarmtz #menopause #tanzaniatiktok #ivfjourney