@salmasaid_znzyetu: PART ONE: Abu Muslim Al Bahalani jina lake kamili ni Nasser bin Salim Al Rawahi alikuwa mshairi, mwanazuoni, na mwanahabari na mwandishi wa vitabu mbali mbali vya fasihi na akida kutoka Nchini Oman. Abuu Muslim anachukuliwa kama mmoja wa watu wenye ushawishi mkubwa katika historia ya Kiswahili na Uarabu wa Afrika Mashariki, hasa kwa kazi yake nchini Zanzibar. Amepata sifa kubwa kutokana na kazi zake za uandishi ametambuliwa kimataifa huko Oman katika watu watatu wanaotambuliwa kuwa ni washairi wakubwa na maarufu mmoja wapo ni yeye Abu Muslim Alizaliwa mwaka 1860 katika Bonde la Mahram, Oman, na alifariki mwaka 1920 Zanzibar na alizikwa makaburi ya Waarabu Rahaleo kwenye msikiti wa Jamia ya Waarabu miaka miwili baada ya kufariki rafiki yake mkubwa Sheikh Rashid Bin Slim Bin Salum Al Ghaithiy aliyekuwa akiishi Mwera Kiongoni. Asili na Elimu: Alikulia katika mazingira ya kidini na kisomi; baba yake alikuwa Qadhi (hakimu) na mwanazuoni wa Ibadhi. Alisoma Quran na Sheria ya Kiislamu kwa wanazuoni maarufu. Akiwa na umri wa miaka 18, alihamia Zanzibar na baba yake mwaka 1878. Kazi Zanzibar: Alihudumu kama Qadhi Mkuu (Hakimu mkuu) kwa Masultani kadhaa wa Zanzibar, akishauri watawala kama Sultani Hamad bin Thuwaini na Hamoud bin Mohammed. Utumishi wake katika mahakama uliisha mwaka 1907 kwa shinikizo la serikali ya kikoloni ya Uingereza. Baba wa Uandishi wa Habari wa Omani: Mwaka 1911, alianzisha gazeti la Al-Najah Zanzibar. Hili lilikuwa jarida la kwanza la kisasa kwa Omani, likitoa mwangaza wa matukio ya kisiasa na kijamii katika ukanda wote wa Ghuba ya Uajemi na Afrika Mashariki. Mwaka 2019, Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) lilimtambua kama mmoja wa watu wenye ushawishi duniani kwenye kumbukumbu ya miaka 100 tangu kifo chake, kwa juhudi zake za kuleta mageuzi kwa njia ya mashairi na uandishi. Ushairi na Wanazuoni: Mbali na kuhudumu kama hakimu, alikuwa na "Madrasa" ya kufundishia lugha ya Kiarabu. Alitoa mchango mkubwa katika fasihi kwa kuunganisha mawazo ya Ibadhi (Fikra ya Kiislamu inayojulikana kwa msimamo wake wa wastani) na Fikra ya Kisufi (Sufi), jambo ambalo lilikuwa la kipeo kwa wataalamu wa Ibadhi nyakati zake. Fahari ya Zanzibar
Salma Said
Region: TZ
Thursday 11 June 2026 13:36:58 GMT
Music
Download
Comments
🌴Albajoun🌴 :
Mashallah nimemuona Sheikh wang Ostadh Salum bin Hemed amepita kweny camera🌹🌹🌹
2026-06-11 20:35:30
4
Mohammed Azan :
Ma'elf ya rehema na nuru ziwe juu yke na ALLAH 🤲 amuingize katika pepo yake pana
2026-06-12 10:49:52
2
ladyhoney :
Maa shaa Allah, Assamadiya nimekisoma kina na mambo ya tiba pia kwa kutumia Habbar sauda nk
2026-06-12 18:02:39
1
Seif Al~jahury :
Allah amrahamu
2026-06-12 21:04:11
1
Redrose🍎🍒 :
: mashallah mungu amrehem mzee wetu
2026-06-13 07:01:19
1
zanzibar ❤️ :
MashaAllah
2026-06-12 05:00:11
1
ALNABHANI :
Maashaallah Allah
2026-06-12 10:31:21
1
el_rawahy007 :
Allah amrehem kaka anguuu
2026-06-12 10:47:12
1
laith :
mashallah
2026-06-12 10:42:52
1
️Farhat Alrawahy :
mashallah mungu amrehem mzee wetu
2026-06-12 13:01:21
1
Halima Suleiman Abdallah :
mash allh
2026-06-11 18:26:34
2
عبدالله :
نسأل الله أن يرحمه ويغفر له ويسكنه فسيح جناته
2026-06-14 18:10:44
0
idris Shariff :
Mashaallah shukran kwa TAREKH
2026-06-11 21:01:46
1
Ismail Van Persie :
MashAllah
2026-06-11 18:51:53
1
NIDAAUN (wito) :
Allah akubarik na akulipe kheir
2026-06-11 18:28:48
1
p53 :
mashallah Mashallah 🥰
2026-06-11 19:01:46
1
هرولة :
هذه هي الأغاني الناجحة القصص التي نريدها
2026-06-12 13:10:56
1
user8127745494751 :
Mashaallah tumejifunza
2026-06-11 17:38:32
1
ruweha :
Alhamdu lilah mashaalwa rehma na Amani yaa rab
2026-06-15 08:31:24
0
مي مي مي :
mashallah
2026-06-12 03:43:18
0
Abdalla Faki :
maashallah dada allah akulipe kwa hili na jengine na jengine
2026-06-12 02:39:33
1
Hamoud Badru Hamoud :
Namuona marehem babu yako hapo juu mama
2026-06-11 18:55:49
1
Ali Seif Salami Al Riyami :
HIZO NDIO HISTORIA ZETU ZNZ NCHI HII INA NEEMA NYINGI ZA HISTORIA💚
2026-06-11 19:28:38
2
Suk :
🥰🥰🥰
2026-06-12 11:24:50
1
khamis :
🥰🥰🥰
2026-06-11 14:05:50
1
To see more videos from user @salmasaid_znzyetu, please go to the Tikwm
homepage.