@dr.sophiak: Ofisi yetu mara kwa mara imekua ikipokea malalamiko kutoka kwa wananchi mbalimbali hasa VIJANA, wakilalamikia kunyimwa mikopo na taasisi rasmi kama mabenki. Lakini baada ya ufuatiliaji tukagundua tatizo kubwa ni MIKOPO YA KWENYE SIMU ambayo wamekopa na kutokuilipa ndio imesababisha wakakosa sifa ya kupata mikopo kwenye taasisi kama mabenki. Ni vyema elimu hii ikawafikia wengi!