@kanikibrown: Mtoto Faith Shao amesema matumizi yake ya simu yanakuwa chini ya uangalizi wa wazazi kupitia mifumo ya kudhibiti maudhui anayoyaangalia mtandaoni. Akizungumza katika Kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 leo Juni 16, 2026, Faith amesema hupenda kufuatilia vipindi vya burudani na podcast kwa ajili ya kujifunza na kujiburudisha. Aidha, amesema ana vipaji mbalimbali ikiwemo uigizaji, uchoraji, mitindo na ushonaji. Faith pia ameeleza kuwa amejikita katika shughuli za biashara akiwa na ndoto za kufanya vizuri katika tasnia anayoipenda. “Ninatamani nikikua niwe Faith anayejulikana na anayefanya vizuri katika tasnia yake,” amesema Faith. #WEWENIFAMILIA Ripota wa Habari za Mikoani ✍ @kaniki_brown “Endelea kufuatilia #Ripotawahabarizamikoani kwa taarifa sahihi na za uhakika. KWA MATANGAZO YA BIASHARA NA HABARI Follow kwa updates zaidi. Kuwasiliana 📞 0622 732 287 #kanikibrown”