@jamiivoice_: Bungeni: Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma amewaonya baadhi ya wabunge wa Zanzibar kujiepusha na kauli na mijadala inayoweza kuleta mgawanyiko na kuhatarisha Muungano wa Tanzania. Musukuma ametoa onyo hilo leo bungeni alipokuwa akichangia mjadala kuhusu Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka wa fedha 2026/2027 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Amesema viongozi wanapaswa kuwa waangalifu wanapozungumzia masuala ya Muungano ili kulinda umoja na mshikamano wa Watanzania. Mbunge huyo pia amemuomba Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi kuchukua hatua dhidi ya mawaziri na wabunge wanaodaiwa kutoa kauli zenye viashiria vya ubaguzi.