@malkiachoicefm102.5: Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Njombe kupitia Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA), Sigrada Mligo, amesema anaona Bajeti Kuu ya Serikali iliyowasilishwa haina sehemu inayoonyesha moja kwa moja kumlenga mwananchi katika maeneo muhimu. Akizungumza na Malkia Choice FM, Mhe. Mligo amesema takribani asilimia 80 ya ongezeko la kodi limeelekezwa kwenye kodi zisizo za moja kwa moja (indirect taxes), ambazo amesema mara nyingi huathiri wafanyabiashara na hatimaye gharama za maisha kwa wananchi. Amesema ni muhimu kuangalia namna sera za kodi zinavyoweza kuleta uwiano kati ya kuongeza mapato ya Serikali na kulinda uwezo wa wananchi kumudu maisha. #MalkiaUpdates #MalkiaChoiceFM #ChaguoLaMalkia