@ndakatv: Mume wa mfanyabiashara maarufu Zari The Boss Lady, Shakib Cham, amedai kuwa bado yupo kwenye ndoa na mkewe, akikanusha taarifa zilizosambaa hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa wawili hao wameachana. Shakib amesema kuwa taarifa hizo si za kweli na kusisitiza kuwa uhusiano wao bado upo imara licha ya tetesi zinazoendelea kusambaa mtandaoni.