@uhondo.tv: Mbunge wa Mbeya Mjini, Patrick Mwalunenge, amesema sekta isiyo rasmi inayojumuisha bodaboda, bajaji na machinga ina uwezo mkubwa wa kiuchumi na inaweza kushiriki moja kwa moja katika kuchangia maendeleo ya miundombinu nchini ikiwemo ujenzi wa barabara. Akichangia mjadala wa Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2025 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, Mwalunenge amesema makundi hayo hayapaswi kuonekana kama maskini bali ni sehemu muhimu ya uchumi wa taifa. #UhondoTVUPDATES