@ngasatvdodoma: Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, Fagason Aron, amewasili Bungeni jijini Dodoma akiwa ameongozana na watoto wake 15, huku mtoto wake wa mwisho akiwa na umri wa miaka sita. Akizungumza na waandishi wa habari, Aron amesema kuwa tangu akiwa mtoto alikuwa na ndoto ya kuwa na familia kubwa, na kwamba alipata mtoto wake wa kwanza akiwa na umri wa miaka 17. Mbunge huyo ameeleza kuwa bado anatamani kuongeza idadi ya watoto wake na kufikia watoto 20 endapo Mungu atamjalia afya na maisha. “Tangu nikiwa mdogo nilikuwa na ndoto ya kuwa na watoto wengi. Kwa sasa nina watoto 15 na kama Mungu akipenda natamani kufikia watoto 20,” amesema Aron. Una maoni gani? Cdt @yasiningitu Kwa Huduma ya Matangazo ya Biashara Dodoma ili uweze Kupata wateja wengi zaidi Piga Simu 0716909567 @ngasamedia_dodoma