@wizara.ya.ardhi: MMUYA ATAKA WAMILIKI WA ARDHI KULIPA KODI YA PANGO LA ARDHI KWA WAKATI KUEPUKA RIBA YA ASILIMIA 1 Arusha
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Kaspar Mmuya, ametoa wito kwa wamiliki wote wa ardhi nchini kuhakikisha wanalipa Kodi ya Pango la Ardhi kwa wakati ili kuepukana na faini na adhabu zisizo za lazima.
Akizungumza leo, tarehe 20 Juni 2026, katika kikao kazi kilichowakutanisha wananchi wa Wilaya ya Arusha pamoja na wataalamu wa ardhi wa Mkoa wa Arusha kwenye Ukumbi wa Hazina Ndogo, Mhe. Mmuya amesisitiza kuwa serikali haitafanya mzaha na mtu yeyote atakayekiuka matakwa ya sheria hiyo.
Mhe. Mmuya ameweka wazi kuwa kila Mtanzania anayemiliki ardhi kihalali ana wajibu wa kisheria kulipa Kodi ya Pango la Ardhi. Aidha, amewaonya wale wanaotumia kisingizio cha kutofahamu sheria ili kukwepa wajibu huo.
"Kutokufahamu si kinga ya kutoadhibiwa. Sheria zetu zimeweka kipengele hiki wazi, na ukienda kinyume unaonekana ni mzembe tu. Sitaki niwaingize kwenye eneo hilo la kusema hamkufahamu," alisema Naibu Waziri Kaspar Mmuya.
Naibu Waziri amefafanua utaratibu wa ulipaji wa kodi hiyo kwa mwaka wa fedha, akibainisha kuwa wamiliki wote wa ardhi wanatakiwa kulipa kodi zao ndani ya miezi sita ya kwanza ya mwaka wa fedha bila kuongezewa riba au faini yoyote. Hata hivyo, mmiliki yeyote ambaye atakuwa hajalipa kodi yake baada ya kipindi hicho ataingia rasmi katika hatua ya kutozwa penalti, ambapo atakatwa riba ya asilimia moja (1%) kila mwezi kulingana na kiasi anachodaiwa.
Ili kuondoa malalamiko na mkanganyiko miongoni mwa wananchi, Mhe. Mmuya amebainisha kuwa vigezo vitatu vikuu vinavyotumika kupanga viwango vya Kodi ya Pango la Ardhi ni ukubwa wa eneo, matumizi ya ardhi pamoja na eneo ilipo ardhi husika (location).
WIZARA YA ARDHI
Region: TZ
Sunday 21 June 2026 13:52:00 GMT
Music
Download
Comments
focusman63 :
kodi nyingiii ila maendeleo sasa 0
2026-06-22 04:50:02
108
Ⓐ︎Ⓜ︎ :
Hii nchi njaa njaa sana
2026-06-21 19:21:06
49
vaydepretyvaydepr :
kwani kodi ya pango si inakatwa kwenye umeme?
2026-06-22 09:20:35
35
walikukunazi :
Natamani kulipa ila na nyie mtupatie hati zetu mapema, tunasumbuka sana
2026-06-21 14:12:16
33
St kitengo :
UKOLONI NI NINI???
2026-06-21 14:57:47
26
rey :
silipi na hakuna kitu mtafanya
2026-06-22 06:42:58
13
Temi :
kwa kutaka kodi tu hamjambo lakini kutupa hati ndio hamtaki. Tangu 2023 nimeprocess hati sijapata lakini natumiwa message za kulipa tu kodi
2026-06-22 11:16:25
13
malikiarecho :
Ardh niya MUNGU au ni ya Nchi achen zenu MUNGU anawaona ,, basi daini na kodo ya Pumzi aliotoa MUNGU
2026-06-22 11:42:34
7
Khadija Kmwaipaya :
mm sijafaham kulipia jengo au ardhi
2026-06-22 18:27:29
3
papaa :
sasa hii ya umeme ni ya nn
2026-06-22 07:13:27
3
BakaI :
tunalipaje kodi na hati zetu hamtoi.. mwaka umepita tangu niombe ila bila bila
2026-06-21 18:04:36
7
wondergloria123 :
Nashukuru mie mlipaji mzuri sana
2026-06-22 04:51:38
3
side Dickies :
Ile tunaolipia tukilipa umeme ni kodi ya nini naomba kujuwa
2026-06-22 06:59:07
4
Ruu Kidoty🦋✈️ :
mwenye anajua taratibu za upatikanaji wa hati Aniambie jmn
2026-06-22 04:19:19
3
urocke23 :
Sasa kulikuwa na maana gani ya kuwa na uhuru
2026-06-22 13:39:19
3
elia ndosi ndosy :
duh karibu Tanzania Kila kitu ni kod. saiv mpaka kwenye mazao. yan. una Lima wew ata dawa awakuchangii ila wana taka ushuru. 🙌🥺
2026-06-22 10:31:35
1
engineer :
ukoloni maomboleo
2026-06-21 21:33:34
5
BAMIZATZ :
unajiamulia sana bro
2026-06-22 07:51:55
1
Sebastian Godian :
Kwani ardh ni ya serekali au ni ya nan mbn hii nch ni ya moto sana
2026-06-22 11:22:17
4
smart boy 06 :
yule marehemu mungu amlaze mahala pema wallah pana tabu kupata tabu kukosa tabu
2026-06-22 14:48:10
2
maisha plus :
kuna kodi ya majengo kwa lazma tunalipa afu kuna kodi ya ardhi khaaa jamani 🥺🥺🥺
2026-06-22 06:34:57
4
Matambo :
Mimi bado sijaelewa kabisaa yaanii kabisaa
2026-06-22 13:11:52
1
love mosha :
Sasa mtu amemilik arch toka mwaka 70 mzee hajui chochote leo anatumiwa taarifa anadaiwa kodi ya ardhi milion 7 kweli jaman
2026-06-24 06:41:57
1
mamy :
Tunalipia wapi hii
2026-06-22 14:53:49
1
Minael Martin :
mm silipi
2026-06-22 05:56:56
2
To see more videos from user @wizara.ya.ardhi, please go to the Tikwm
homepage.