@millardayo_: Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando amesema hatokubali ongezeko la tozo kwa Maafisa Usafirishaji ‘Bodaboda’ akisisitiza kuwa kundi hilo ni miongoni mwa Vijana waliowahi kuwa msaada mkubwa wakati wa kampeni za uchaguzi. Akizungumza leo Juni 22, 2026 Bungeni Jijini Dodoma katika Bunge la Kumi na Tatu, Kikao cha Hamsini na Nne amesema bodaboda walitumika kama “Jeshi la mbele” katika harakati za kisiasa za kupata ushindi katika majimbo mbalimbali. Ameeleza kuwa wakati wa kugombea nafasi za uongozi alijitambulisha kwa ukaribu na kundi hilo, akisema hata aliwahi kujinasibisha kama ‘Mfalme wa Bodaboda’ hivyo hawezi kukaa kimya kuona Vijana hao wakiongezewa mzigo wa kodi au tozo mpya. “Hatutakubali Vijana waongezewe mzigo, asilimia kubwa ya bodaboda ni darasa la Saba, sehemu walipojiegemeza tunawaangamiza.”
Genius sana 🧠✊🏾 mungefahamu msoto wa kumaliza mkataba wa boda boda wala musingethubutu hata ku mention jina la boda boda kwenye tozo🥹…. Mimi sio boda boda ila naona mitaani what they’ve been through 😔
2026-06-22 18:25:33
2
Ibrahim :
chukua fom kaka unapita🥺🥺
2026-06-22 16:02:31
1
Jose27junior# :
Wahenga hawamini nin kinatokea kwa mhe. baba levo
2026-06-22 16:59:28
1
@puresmile🥰🔥 :
jina nani tutume jina kwa mungu na yy apungue
2026-06-22 19:23:26
0
ceeskippa400 :
kun mda unaongeag fact
2026-06-23 03:14:04
0
kotinyo :
Mke wangu anawivu sana
2026-06-22 18:46:07
0
boraauni :
Kigoma tunajivunia Mwamba huyu 🔥
2026-06-22 19:35:58
0
Zakayo Richard :
hapo hutosikia makofi maana anawapasua vichwa wakandamizaji
2026-06-22 18:00:25
0
To see more videos from user @millardayo_, please go to the Tikwm
homepage.