@bantu_media: Mkaguzi Mkuu na Madhibiti wa Hesabu za Serikali Mstaafu (CAG) Professa Mussa Assad amesema moja ya kosa lililofanyika nchini ni kuruhusu wafanyabiashara kuingia katika siasa kwani kuna wakati wanaruhusu baadhi ya mambo kwani yana maslahi nao. Professa Assad amesema hayo leo Juni 22, 2026 akihojiwa na Clouds TV akieleza kuwa jambo hilo ni hatari. "mimi binafsi nadhani kosa kubwa tulilofanya ni kuruhusu wafanyabiashara kuingia katika siasa. Wakati wa Mwalimu Nyerere kama wewe unahusika na biashara ulikuwa huruhusiwi kuingia katika siasa," amesema Prof. Assad