@okulyjulius: Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa (BMH) imeendelea kuonesha uwezo wake katika utoaji wa huduma za kibingwa baada ya kufanikiwa kuwahudumia wanaume 14 kwa upandikizaji wa uume, huduma iliyoanza kutolewa mwaka 2023. Kaimu Mkurugenzi wa BMH, Dk. Abdallah Baja, amesema hayo wakati akizungumza kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya hospitali hiyo, akibainisha kuwa wagonjwa wote waliopatiwa huduma hiyo wanaendelea vizuri na matokeo ya matibabu yamekuwa ya kuridhisha. Amesema mafanikio hayo yanaakisi maendeleo ya BMH katika kutoa huduma za kibingwa zinazopatikana katika hospitali chache ndani na nje ya nchi.