@vitarcaretz: Usipochukua hatua mapema na kuendelea kupuuza dalili za awali, Hepatitis B sugu inaweza kusababisha madhara makubwa, ikiwemo: 1:Ini kuharibika (Cirrhosis) – Ini hupoteza uwezo wa kufanya kazi vizuri kutokana na makovu ya kudumu. 2;Saratani ya ini – Kuwa na Hepatitis B sugu huongeza hatari ya kupata saratani ya ini. 3:Ini kushindwa kufanya kazi (Liver Failure) – Hali inayoweza kuhatarisha maisha na huhitaji matibabu ya haraka. 4:Kuchanganyikiwa au kuvurugika kwa utendaji wa ubongo – Ini linaposhindwa kuondoa sumu mwilini, sumu zinaweza kuathiri ubongo na kusababisha kuchanganyikiwa, kusahau, usingizi mwingi au hata kupoteza fahamu. 5:Hatari ya kifo endapo matibabu na ufuatiliaji havitapatikana kwa wakati – Madhara makubwa ya Hepatitis B yanaweza kuhatarisha maisha. Kumbuka: Watu wengi wenye Hepatitis B wanaweza kuishi kwa miaka mingi bila madhara haya ikiwa wanagunduliwa mapema, wanafuatiliwa na kupata matibabuu wanapohitajika. Kupata dalili hizi hakumaanishi mtu tayari amefikia hatua hizo, bali ni ishara ya kutafuta huduma za afya haraka. Kama unadalili zaini coment Neno INI nikuonyeshe Njia au coment Dm Neno DALILI nikusaidie #creatorsearchinsights #AfyaYaIni #foryou #villl