@madiniplus_: Wilbard Chambulo anaeleza jinsi vijana wa Kitanzania wanavyofanikiwa kwenye sekta ya utalii kwa kuanza kama madereva na waongozaji watalii, kisha kujiongeza kwa kujenga uaminifu na mahusiano ya karibu na wageni, jambo linalowafanya wapate wateja wa moja kwa moja na hatimaye kumiliki makampuni yao wenyewe ya utalii yenye gari moja au mawili. Aidha, anasisitiza umuhimu wa vijana hawa kujifunza lugha mbalimbali za kigeni kama Kichina na Kijerumani badala ya kutegemea Kiingereza au Kiswahili pekee, kwani ujuzi huo unawapa fursa ya kuajiriwa na kuongeza kipato chao kwa kiasi kikubwa wanapohudumia watalii kutoka mataifa hayo. Video, Clouds Media