@storyhousetz_: Naitwa Neema Chacha, mkazi wa Bunda. Mnamo Desemba 2024 nilikuwa Stendi ya Magufuli – Dar es Salaam nikisubiri basi la kwenda Musoma. Bahati mbaya niliibiwa mkoba wangu uliokuwa na simu na pesa zote, na sikuwa bado nimelipia nauli. Katika wakati huo mgumu, kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la James alinisaidia sana. Aliniombea kwa konda, akanilipia nauli ya shilingi 40,000, akanipa shilingi 15,000 za matumizi, na pia akanipa simu ndogo ya Nokia kwa sababu simu yangu ilikuwa imeibwa. Aliniambia alikuwa akielekea Tarime baada ya kufika Mwanza. Sikupata mawasiliano yake kwa kuwa simu aliyoniachia haikuwa na namba yoyote. Nakumbuka alivaa kofia ya bluu na jezi nyekundu ya Manchester United. Kwa sasa ningependa kumpata ili nimshukuru na kumrudishia fadhila zake. Kama unamfahamu James mwenye maelezo haya au una taarifa zozote zinazoweza kusaidia kumpata, tafadhali nijulishe 07651156781 Wema hauozi. Mungu ambariki sana James popote alipo. ❤️ #swahilitiktok #tanzaniatiktok #tanzaniantiktok🇹🇿 #tanzania #mbeya
HOUSE OF STORY Tz
Region: TZ
Sunday 28 June 2026 14:36:42 GMT
Music
Download
Comments
James ndambile :
I’m here 🥰
2026-07-11 17:06:19
2
Aroon :
James typing
2026-07-11 18:59:33
0
1443james :
am here
2026-07-12 09:34:39
0
Niko hapa saiv naitwa festo nilibatizwa upyaa
2026-07-09 12:51:06
52
mwanafalsafa :
mwanamke wakwanza dunian anaekumbuka fadhila ni wew mungu akutunze sana kwaniaba yangu
2026-06-30 16:54:27
98
midolitz :
na mimi namtafuta rafiki yangu dada yangu Groly Akyoo alikuwa anaishi mbezi anafanya kazi DSTV kinondoni , mi nilikuwa nakaa sinza mlimani city 2018 , dah mpaka leo hatujawasiliana wala kuonana nimekutafuta sana bila mafanikio.Now nipo kinondoni
2026-07-11 15:56:50
3
James Benard :
ametuwakilisha vema aseee
2026-07-12 20:30:04
2
user4813259140858 :
Usimshukuru kwa mapenzi ukaharibu ndoa ya watu
2026-06-28 16:23:11
21
MIS DIAH :
Nd umejipata mwaka huu et
2026-07-12 18:25:48
1
James Godfrey :
Ametuwakilisha vyema, but alikupa kwa moyo wote Mungu ashambariki sana kwa kuwa alichagua baraka kuliko pesa.
2026-07-01 13:52:08
28
Muhaya @og :
nishaoa na mke wangu nampenda sana ACHA na mm bhana
2026-07-12 06:18:25
2
Majays :
Mungu akubariki sana wewe dada...wachache sana huwa wanarudi.
2026-07-12 15:55:37
1
frenki Johni :
machozi yanitoka nimekumbuka mbli
2026-07-09 03:22:12
10
Jimmy wanaman :
ndo mm james apa nakukumbuka mama
2026-07-11 12:48:06
3
Aivanny 🇹🇿🇨🇦 :
🙏🙏 nashukur madam neema kwa kunikumbuka me nipo salama sana ile namba ulionachiaga ilipatikana kwa muda t nashukur kwa shukuran zako ila kwa sasa nilipata kaz nipo nchin canada na nalud mwez 8 nitakuja musuma kukuona
2026-07-01 10:57:05
12
chipo sailor :
nipo apa me apa
2026-07-11 09:12:49
1
Peter Mwasijaga :
mungu akubariki kwa kukumbuka fadhila ni wanawake wachache sana wanaokumbuka ilo mungine angesema nimelichuna au Angejiona ni haki sababu mzuri
2026-07-10 21:29:28
4
currentthomas :
ilikuwa siku ya juma tano mwezi wa 5 ulivaa suruali na tshert niko rorya karibu
2026-06-28 19:53:06
8
Chugastan❤️🔥 :
Good girl nmependa 🥰
kumbe Kuna watu wanajua kulipa fadhila
2026-06-29 03:48:33
9
shiwalee :
nipo hapa mama angu
2026-07-09 10:44:50
1
Edson Kalangali :
Dada Nina mke sasaivi vipi unaendeleaje
2026-07-12 13:40:14
3
bepari Bampenja :
mungu akufungulie nilango James upate Itaji lako
2026-07-08 16:30:31
2
Baraka Iddi Mdee :
kwa uwezo na mapenzi ya mwenyez mungu kwa fadhila mnazotaftana mtakutana tu,nina iman na wa Tz,watakusaidia kwa hilo
2026-07-08 08:39:08
3
Daniel Mwambeje :
nimejikuta nalia kwa furaha, wanawake wachache wenye moyo kama huo,Mungu akukutanishe na Jems
2026-07-10 13:35:31
4
James tz🇹🇿🇹🇿 :
ndo mimi dada yangu nipo zanzibar saa ivi nakaa mta wa aman
2026-07-01 19:35:48
0
To see more videos from user @storyhousetz_, please go to the Tikwm
homepage.