@irenefalifali: Baba katika jina la Yesu Kristo Asante kwa neema yako na nguvu zako Baba ninaomba unisamehe makosa yangu yote niliyotenda mbele zako Ninaomba unijibu maombi yangu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth maana imeandikwa 📖Zaburi 128:2 "Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema. Baba ninakusihi Bariki kazi ya mikono yangu Bariki shamba langu likanipe mazao Bwana Yesu Kila kazi ya mikono yangu ikanipe matunda Nikaifurahie na kuinuka kiuchumi katika jina la Yesu Kristo maana imeandikwa 📖Warumi 8:28 "Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Bwana Yesu Kusudi la kupata kazi nzuri uliloliweka ndani yangi likatimie katika jina la Kusudi la kuinuka kiuchumi likatimie katika jina la Yesu Kusudi la kufanikiwa likatimie katika jina la Yesu Kristo Ninaamuru Kila nguvu za giza inayozuia matunda ya kazi yangu ninaisambaratisha kwa jina la Yesu Kila roho za giza zinazonifatilia ninaziangusha kwa jina la Yesu Kristo Baba ninakuomba maana imeandikwa 📖Kutoka 14:14 "BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. Pigana kila vita iliyoinuliwa kazini kwangu Pigana kila vita iliyoinuliwa kwenye biashara yangu Pigana kila vita iliyoinuliwa kuzuia uchumi wangu kuongezeka katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth Baba katika jina la Yesu Ninaamuru Katikati ya matajiri jina langu litajwe Katikati ya watu wanaojua kufanya kazi ofisini jina langu litajwe Katikati ya watu walioinuliwa jina langu litajwe Katikati ya watu wenye hekima na utajiri jina langu litajwe kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareth mwana wa Mungu alie hai Ninaamuru Nuru yako ing'ae kwenye uso wangu Kibali chako kinifunike na kunitangulia mbele Uchumi wangu hautaangushwa tena katika jina la Yesu Kristo Baba asante kwa kunipa neema na nguvu ya kuomba na kulisoma neno lako katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth mwana wa Mungu alie hai #creatorsearchinsights