@aviationtanzania: Helikopta iliyobeba kombe la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliruka juu ya Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo wakati mchezo wa mwisho wa msimu kati ya Yanga na JKT Tanzania. Kombe hilo hatimaye limekabidhiwa rasmi kwa Young Africans baada ya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa mwisho wa msimu, wa Mwaka 2026. #youngafricans #yangasc #aviationtanzaniaupdates #helicopter #nbcpremierleague