@cawabemedia_: Mahakama ya Rufani imesema itatoa uamuzi wake hivi karibuni baada ya kukamilisha usikilizaji wa hoja za pande zote katika rufaa iliyowasilishwa na Jamhuri, ikipinga uamuzi wa Mahakama Kuu uliokataa ombi la kuwasilisha ushahidi wa nyongeza katika kesi inayomhusu Tundu Lissu. Katika shauri hilo, Jamhuri imeiomba Mahakama ya Rufani kutengua uamuzi wa Mahakama Kuu ili iruhusiwe kuwasilisha ushahidi huo wa nyongeza, huku upande wa utetezi ukitetea uamuzi wa mahakama hiyo. Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, jopo la majaji limeahirisha shauri na kueleza kuwa uamuzi wake utatolewa hivi karibuni.