@muhammadfacky: Usichanganye ushahidi wa mauziano na hati ya umiliki. Barua ya Serikali za Mitaa inaweza kuthibitisha kuwa mauziano yalifanyika, lakini haitoi haki ya umiliki wa ardhi kama hati ya umiliki inayotolewa kupitia mamlaka za ardhi. Kabla hujanunua kiwanja au shamba: ✅ Hakikisha unajua hadhi ya eneo. ✅ Hakikisha nyaraka zake zimehakikiwa. ✅ Elewa kama eneo lina hati au linaweza kupatiwa hati kwa mujibu wa sheria. Elimu ya sheria leo inaweza kukuokoa dhidi ya hasara kesho. #ardhi #realestate #businesstips #businessgrowth #legal