@paza_sauti_media: Amos Hamis, kijana aliyekuwa akijihusisha na vitendo vya ushoga na aliyefahamika kwa jina la 'Aunt Asu', katika mahojiano maalum na Paza Sauti Media, amesema amebadilika kitabia na kuamua kuokoka na kuwa mfuasi wa Yesu Kristo. Amos ameazimia kuhubiri Injili kupitia kipawa chake cha uimbaji ili kuwafikia vijana wengi wanaojihusisha na vitendo kama hivyo, akiwahimiza kuviacha na kumtumaini Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa maisha yao. Amesisitiza kuwa vitendo hivyo vinapaswa kuepukwa. Amos pia ameiomba Serikali pamoja na taasisi mbalimbali kumuunga mkono katika juhudi zake za kutoa ushuhuda na kuwa balozi wa kuwasaidia watu waliopotea kurejea kwenye mwenendo unaokubalika na unaoendana na maadili Tanzania. NB: Yafuatilie Mahojiano hayo yapo YouTube Paza Sauti Media