@samir_abed_: Maqam (mahali pa heshima/kumbukumbu) ya Sayyidna Bilal huko Damascus. Je, unajua mapenzi ni nini? Mapenzi ni Sayyiduna Bilal kukataa kutoa Adhana baada ya Rasulullah (s.a.w) kufariki dunia, kwa sababu hakuweza kustahimili kuitoa bila kuuona uso wake mzuri. Na mapenzi ni Sayyiduna Bilal kuondoka Madinah na kuhamia Syria, kwa sababu kila kitu Madinah kilimkumbusha Mtume (s.a.w), na hakuweza kuishi katika mji huo bila kumuona Rasulullah (s.a.w) kila siku. Na mapenzi ni Sayyiduna Bilal alipozuru madina na kuombwa apige adhana na alipofikia sehemu ya kumtaja mtume Muhammad (s.a.w) ile “Ashhadu anna Muhammadan Rasulullah (s.a.w)…” alipasuka kwa kilio, na Maswahaba wote wakalia pamoja naye mpaka ndevu zao zililowa kwa machozi. Kwa nini? Kwa sababu katika siku yao ya furaha kubwa kabisa, mioyo yao ilikuwa imevunjika kwa huzuni kuwa furaha hiyo haingeweza kuishiwa pamoja na Rasulullah (s.a.w). Na mapenzi ni Sayyiduna Bilal alipokuwa katika kitandacha mauti akisema: “Ni siku iliyojaa furaha iliyoje! Kesho ni siku ya kukutana na Muhammad (s.a.w) na Maswahaba wake!” Usiondoke bila kunifollow naomba