@veriafya: Kupitia mahojiano aliyofanya na Veriafya, Daktari Bingwa wa Masikio, Pua na Koo, Costancia Kilawe anaeleza kuwa ngono ya mdomo (oral sex) ni tabia iliyozoeleka kwa vijana na watu wazima, lakini si salama na inaweza kusababisha hatari ya kupata saratani ya koo. Anafafanua kuwa watu wenye wenza wengi wa ngono wanaweza kubeba virusi vya HPV kwenye viungo vyao vya uzazi na wanapofanya ngono ya mdomo, virusi hivyo huhamia na kubaki kwenye koo ambapo huzaliana na kuleta saratani hiyo, hivyo hashauri kabisa tabia hiyo kwa usalama wa koo.