Alwattan 20 :
🤔 Dah! Kwa kweli, watu wa Zanzibar wamechoshwa na hila, fitina na ahadi zisizotekelezwa za kila siku. Katika nyakati kama hizi, si rahisi kumpata mtu anayesimamia maslahi ya watu kwa moyo wa dhati, uadilifu na usawa bila ubaguzi.
Kwa yote unayoyafanya kwa nia safi na kwa kutanguliza maslahi ya watu, hakuna malipo ambayo watu wanaweza kukulipa yanayolingana na thamani ya juhudi zako. Malipo ya kweli yanatoka kwa Allah, ambaye halipotezi jema la mwenye kufanya mema 🥰 .
🤲 Allah akulipe kheri nyingi, akubariki katika maisha yako, akuzidishie afya njema, hekima, busara, subra na tawfiki. Ajaalie kila hatua unayoichukua kwa ajili ya haki, uadilifu na usawa iwe katika mizani ya mema yako duniani na Akhera. Allah akulinde dhidi ya kila shari, akuongoze katika kila jambo jema na aendelee kukutia nguvu ya kuwatumikia watu kwa ikhlasi. Ameen Yaa Rabbal Alamiina . 🤲
2026-07-09 19:56:45