@akhi_ali5: Upeo wa akili huanza pale unapotambua kuwa hakuna aliye msafi. Sote tunabeba mapungufu yetu; tofauti ni kwamba mara nyingi tunaficha yale yanayotupendeza na kuyaona madogo, huku tukiyakuza makosa ya wengine kana kwamba sisi hatujawahi kukosea. Hekima ya kweli haipo katika kuwahukumu watu, bali katika kuinyenyekeza nafsi, kujitathmini, na kuwatendea wengine kwa huruma ile ile tunayotamani tutendewe. #creatorsearchinsights #viralvideo