@massoudkhaifan: Kusamehe si rahisi, hasa pale ambapo maumivu yalitoka kwa mtu uliyemwamini kwa moyo wote. Mara nyingi anayesamehe haimaanishi kwamba amesahau, bali amechagua kuachilia maumivu ili moyo wake upate amani. Kuna machozi ambayo hayamwagiki, kuna majeraha ambayo hayaonekani, na kuna hisia zinazobaki kimya kwa sababu si kila maumivu yanahitaji kulipiziwa. Wakati mwingine, msamaha si zawadi kwa aliyekuumiza, bali ni zawadi unayojipa mwenyewe ili usiendelee kubeba mzigo wa maumivu moyoni. 🤍🥀 #mahdankhaifan #fypage #fyp #viral