@enockchristopher5: "YESU AKIWA NA SHOW, WATAKUJA KUJIFUNZA" — MATAMANIO YA MTUMISHI WA MUNGU KUTOKEA ARUSHA Moja ya matamanio makubwa ya wachungaji wengi ni kuona huduma ya Mungu ikisonga mbele kwa kasi na kulijenga kanisa la Kristo kwa viwango vya juu. Kauli hii imekuja kufuatia ujumbe mzito kutoka kwa mtumishi wa Mungu anayepatikana jijini Arusha, ambaye amegusa mioyo ya wengi kwa kusema: "Yesu akiwa na show, watu watakuja kujifunza." Je, nini maoni yako juu ya kile alichokizungumza mtumishi huyu wa Mungu kutoka jijini Arusha? Unadhani anamaanisha nini hasa? Karibu sana kwenye uwanja wa maoni (comments). Usisahau kulike ujumbe huu, na pia tembelea chaneli yetu ya YouTube ya Stein TV. Tafadhali subscribe na kulike video zetu ili uwe wa kwanza kupata habari mbalimbali moja kwa moja kwenye kiganjani mwako! #SteinTV #SaayaUshuhuda
Kitu cha kwanza mtu anaenda kwa ajili ya vitu vizuri au unaenda kwa ajili ya Neno la MUNGU ukiona mtu anaenda kwa ajili ya vitu vizuri hajamfuata MUNGU kwa sababu ya Neno bali amemfuata YESU kwa sababu ya mikate, na YESU aliwambia watu kama hao aliwaambia amnifuati kwa sababu ya Neno nililowaambia bali mnanifuata kwa sababu ya mikate kwa hiyo hakufanya tena muujiza wa kushusha mikate, na katika nyakati za kale wakati walikuwa wakifundisha mahubiri yao tumwangalie YESU KRISTO ambaye ni kielelezo yeye alihubiri aliketi kwenye mtumbwi tena baharini aliketi nyikani wala akutengeneza majukwaa wengine walimfuata Yohana Mbatizaji walimfuata naye nyikani wala akutengenezea majukwaa muda mwingine YESU aliacha mahekalu alienda na kuhubiri njiani na watu walilipokea Neno kwa hiyo sisi hatuwaigi mataifa ninaposema mataifa maanake wasioamini sisi tunamuiga YESU KRISTO MWOKOZI WETU.
huyo diamond ni nani mimi hata niiga njia zake njia zilizopotoka njia za anasa zisizompendeza MUNGU siwezi nikaiga njia zake yeye anatakiwa kuiga njia zetu anyenyekee na akimfata MUNGU ROHO MKUU MTAKATIFU, Aishiye Milele.
2026-07-20 09:45:15
0
Prosper Jackson :
ata mimi mwenyew nataka vizuri vianze kanisan
2026-07-14 11:27:50
0
Prof John Mshanga :
hakika nikweli watu wengi hufuata vitu vizuri kwenye maeneo ya mambo ya kidunia kuliko kwa yesu ni kwasababu pia fahamu zetu na mapokeo yametufunga sana wakristo wengi tunaamini vizuri ni vya shetani lakini sio vyote vipo vizuri vinavyomtukuza Mungu ambavyo vinafaa kuwavutia vijana na kumuelewa yesu zaidi
2026-07-14 09:44:59
0
amosi :
amen
2026-07-14 13:41:11
0
To see more videos from user @enockchristopher5, please go to the Tikwm
homepage.