@miladu_tv: Baraza la BAKWATA limeazimia kuwasimamisha Masheikh wa Mikoa mitatu kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni mienendo inayokiuka misingi ya kiuongozi ya Baraza hilo. Baraza hilo limekutana leo Julai 14, 2026 katika kikao cha dharura kilichoongozwa na Kaimu Mufti na Naibu Kadhi Mkuu wa Tanzania, Sheikh Ally Khamisi Ngeruko na kuazimia kuwasimamisha Masheikh hao. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Hassan Said Chizenga, Masheikh waliosimamishwa ni Sheikh Walid Alhad Kawambwa wa Mkoa wa Dar es salaam, Sheikh Issa Nassor Issa wa Mkoa wa Singida pamoja na Sheikh Hassan Kiburwa wa Mkoa wa Kigoma. Taarifa hiyo imeeleza kuwa utekelezaji wa maamuzi hayo unaanza rasmi leo Julai 14, 2026. Aidha, Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir Mbwana, amewateua Viongozi wa muda kushika nafasi hizo hadi pale hatua nyingine zitakapochukuliwa. Waliopewa nafasi hizo za Ukaimu ni Sheikh Abasi Ramadhani Abasi ambaye atakuwa Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam, Sheikh Issa Ramadhani Simba aliyeteuliwa kuwa Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Singida na Sheikh Uwesu Mohamed Kiumbe ambaye atahudumu kama Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Kigoma. BAKWATA pia imeielekeza Ofisi ya Katibu Mkuu kusimamia makabidhiano ya ofisi hizo ndani ya muda mfupi. @miladu_tv #babdeoMiladu #MiladuUpdates
Babdeo Miladu
Region: TZ
Tuesday 14 July 2026 13:44:55 GMT
Music
Download
Comments
mjbackup :
NACHOJUA MIMI NI KWAMBA SHEKHE WALID NI MOJA YA WANADAMU WAKIPEKEE SANA NA AMEBARIKIWA KUPENDWA NA NI KIONGOZI WA WATU HILI HALITABADILIKA KAMWE.ALLAH AMJAALIE MTU HUYU WA WATU KHERI NYINGI INSHAALLAH 🙏🏻
2026-07-14 15:19:04
52
Madrasatu Al-wahhaab :
Unaweza ukalichukia jambo kumbe nikheri kwako. na unawaeza ukalipenda jambo kumbe nishari kwako. sikuzote sema Alhamdulillah
2026-07-14 14:50:20
25
prencerateo :
waislam wameumia sana
2026-07-14 15:07:26
34
yusuphutuji :
Allah atunusuru
2026-07-14 15:04:58
1
remmyshalismohamm :
itakua wamechunguza wakaona ni kweli kuhusu sheikh walid
2026-07-14 16:01:02
8
Rwambo :
weka sababu hapo
2026-07-14 16:05:16
3
MAJINA MENGI 💫🫰 :
shekhe wardi mnamsimamisha kivipi mnauhakika na kinachoelendele kwenye mitandano duh 😭
2026-07-14 15:43:52
5
pilipili :
jmn tuna mpenda shekh wetu plz
2026-07-14 16:08:51
0
MENEJA SUMA :
shekhe Walid mmemuonea sisi kama waislamu Bado tupo nae
2026-07-14 15:47:45
9
Golden saw :
hizo sababu mbona hamzitaji ss
2026-07-14 14:33:54
18
user6176312472429 :
wasameheni jamani ,kutenda kosa sio kosa bali kuludia kosa ndio kosa,nawaombea msamaha muwasamehe jamani 😭
2026-07-14 16:02:23
1
Rukhal Rukhi :
mungu ndo anajua ukweli zaid kama kuna khila yyote Allah ataibainisha mbele ya umma inshallah
2026-07-14 15:46:01
4
Chanukah :
I'm proud to be Muslim
2026-07-14 15:36:53
0
mister counsellor :
mbona wamekimbilia kumsimamisha ghafla
2026-07-14 14:13:52
7
yasini mbembati :
Hakika huu ndio uislamu dini ya haki isiyofumbia macho uovu wowote
2026-07-14 16:04:41
4
MAHIBU 55 👑🍀🍁 :
mungu akupe uvumilivu sheakh walid kpnz ch waisilamu
2026-07-14 16:36:40
1
محمد بن صالح العثيمين :
hapo kuna Siri sheikh walidi aliashiriwa kupewa umufti nadhani muda umefika
2026-07-14 15:40:35
1
🔵 Ismail Care TZ ✔️ :
Hili lilisukwa ndo maana imekuwa harakaharaka ivyo kabla mambo hayajapoa😅
2026-07-14 16:25:55
1
Chisokole LM :
Nimeumia sana, sheikh Walid, Allah akupe uvumilivu.
2026-07-14 16:24:32
1
Amina Ali :
hila tu tunajuwa kama ni michezo mmefanya😭😭😭😭😭😭
2026-07-14 15:31:21
4
𝐏𝐎𝐊𝐎𝐌𝐎 𝐕𝐈𝐁𝐄𝐒 🇰🇪 :
Sheikh Walid tunamhitaji ...bado hamja tupatia sababu ya kusimamishwa
2026-07-14 15:44:59
2
DIDAH DIDAH :
Itakuwa ni funzo kwa ma sheikh wengine
2026-07-14 15:54:04
3
Altiwany :
tangu zamani nilisema hapo hakuna shekh
2026-07-14 15:21:50
3
Kijana wa Iran :
Walid ndo tunamtaka sisi
2026-07-14 15:54:18
0
mamsap :
ila jamani shekh wetu baadae atakuwa mufti inshallah ☺️
2026-07-14 14:56:55
4
To see more videos from user @miladu_tv, please go to the Tikwm
homepage.