@atuganilemwakosya: YESU SASA NAKUTAKA, NAAMUA KUTUBU DHAMBI Kauli hiyo ilisikika kutoka kwa mlevi aliyejikuta akihubiri Injili kwa hisia kubwa, akiwataka watu wamgeukie Mungu na kuacha maisha ya dhambi. Tukio hilo limewagusa wengi na kuzua mijadala mitandaoni, huku baadhi wakisema linaonyesha kuwa Mungu anaweza kumgusa mtu kwa namna yoyote na wakati wowote. Wengi wamekumbusha kuwa neema ya Mungu inamfikia kila mtu, bila kujali historia yake, na kwamba toba ya kweli ndiyo mwanzo wa maisha mapya ndani ya Kristo.