@cali_omz: Ndugu yangu. Kama leo uko kisimani… Usikate tamaa. Kama leo uko kwenye gereza la matatizo… Usikate tamaa. Kama watu waliokuumiza ni wale uliowaamini… Usikate tamaa. Kwa sababu Mola wa Yusuf bado ni Mola wako. Mwenye kugeuza kisima kuwa ikulu bado yupo. Mwenye kugeuza machozi kuwa furaha bado yupo. Mwenye kugeuza maumivu kuwa ushuhuda wa rehema zake bado yupo. Na mwisho wa kisa hiki Allah anatupa ujumbe ambao kila mwenye huzuni anatakiwa auandike moyoni: “Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na ndugu yake, wala msikate tamaa na rehema ya Allah. Hakika hakuna anayekata tamaa na rehema ya Allah isipokuwa watu waliokufuru.” (Surah Yusuf: 87) #Fyp #islamic_video #surahyusuf #daawah