@fredhuman_care: SABABU 5 ZA ACID REFLUX (GERD) 1.Kula chakula kingi kwa wakati mmoja – Huongeza shinikizo tumboni na kufanya tindikali irudi kwenye umio. 2.Vyakula vyenye mafuta mengi – Hupunguza kasi ya tumbo kumeng'enya chakula na kulegeza misuli inayozuia tindikali kurudi juu. 3.Unene uliopitiliza – Huongeza shinikizo ndani ya tumbo na kuchochea acid reflux. 4.Kulala mara tu baada ya kula – Hufanya tindikali iwe rahisi kupanda kutoka tumboni kwenda kwenye umio. 5.Uvutaji wa sigara na unywaji wa pombe – Hulegeza misuli ya chini ya umio (Lower Esophageal Sphincter), hivyo kuruhusu tindikali kurudi juu. 👉Acid Reflux si jambo la kupuuza. Kubadili baadhi ya tabia za maisha kunaweza kusaidia kupunguza dalili kama kiungulia, ladha chungu mdomoni, na maumivu ya kifua. Ukiwa na dalili zinazojirudia mara kwa mara, ni muhimu kufanyiwa uchunguzi na kupata ushauri wa daktari. #AcidReflux #GERD #AfyaYaTumbo #FredhumanCare #ElimuYaAfya