@devovibes: slimfit tanks overly crispy😮‍💨 #foryou #devovibes #tanktops

devo💲
devo💲
Open In TikTok:
Region: US
Sunday 19 July 2026 00:22:35 GMT
272
7
1
0

Music

Download

Comments

secretspiderman27
🕷️🕸️man :
First
2026-07-19 03:34:57
0
To see more videos from user @devovibes, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos

Hali ya sintofahamu imejitokeza katika Kijiji cha Ibondo, Kata ya Ludete, wilayani na mkoani Geita, baada ya ng’ombe wanne kutoka Kata jirani ya Kaseme kukutwa wamekufa kwa madai ya kula chakula chenye sumu kilichokuwa kimetegwa ndani ya shamba la mkulima. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ibondo, Bw. Cornel Lupimo, amesema tukio hilo limetokea Julai 17, 2026, na kulaani kitendo hicho alichokitaja kuwa cha kinyama na kinachoweza kuhatarisha amani na usalama wa wananchi. Kutokana na tukio hilo Bw. Lupimo ametoa wito kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi, badala yake kutumia vyombo vya serikali za vijiji na mamlaka husika katika kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza kati ya wakulima na wafugaji. Kwa upande wao, wamiliki wa mifugo hiyo, Bw. Mapambano Ndegea na Bw. Sizya Ndegea, wamesema walifika eneo la tukio na kukuta ng’ombe wanne tayari wamekufa, huku wengine wakipewa matibabu ya awali katika jitihada za kuwanusuru. Wafugaji hao wameeleza kuwa wanahisi tukio hilo linaweza kuhusishwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji, wakidai kuwa baadhi ya wakulima huenda wakahusika na tukio hilo. Aidha, wameiomba serikali kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya shughuli za ufugaji ili kupunguza na hatimaye kumaliza migogoro hiyo. Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnekezi, Kata ya Kaseme, Bw. Ferisian Mlazi, amelipinga vikali tukio hilo akisema kuwa matumizi ya sumu katika mazingira ya wananchi ni hatari kubwa, kwani vinaweza kuhatarisha maisha ya binadamu, hususan watoto wadogo ambao wangepita katika eneo hilo. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kaseme, Mhe. Andrea Karamla, amewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu na kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga amani wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
Hali ya sintofahamu imejitokeza katika Kijiji cha Ibondo, Kata ya Ludete, wilayani na mkoani Geita, baada ya ng’ombe wanne kutoka Kata jirani ya Kaseme kukutwa wamekufa kwa madai ya kula chakula chenye sumu kilichokuwa kimetegwa ndani ya shamba la mkulima. Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Ibondo, Bw. Cornel Lupimo, amesema tukio hilo limetokea Julai 17, 2026, na kulaani kitendo hicho alichokitaja kuwa cha kinyama na kinachoweza kuhatarisha amani na usalama wa wananchi. Kutokana na tukio hilo Bw. Lupimo ametoa wito kwa wananchi kutojichukulia sheria mkononi, badala yake kutumia vyombo vya serikali za vijiji na mamlaka husika katika kutafuta suluhu ya migogoro inayojitokeza kati ya wakulima na wafugaji. Kwa upande wao, wamiliki wa mifugo hiyo, Bw. Mapambano Ndegea na Bw. Sizya Ndegea, wamesema walifika eneo la tukio na kukuta ng’ombe wanne tayari wamekufa, huku wengine wakipewa matibabu ya awali katika jitihada za kuwanusuru. Wafugaji hao wameeleza kuwa wanahisi tukio hilo linaweza kuhusishwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya wakulima na wafugaji, wakidai kuwa baadhi ya wakulima huenda wakahusika na tukio hilo. Aidha, wameiomba serikali kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya shughuli za ufugaji ili kupunguza na hatimaye kumaliza migogoro hiyo. Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Mnekezi, Kata ya Kaseme, Bw. Ferisian Mlazi, amelipinga vikali tukio hilo akisema kuwa matumizi ya sumu katika mazingira ya wananchi ni hatari kubwa, kwani vinaweza kuhatarisha maisha ya binadamu, hususan watoto wadogo ambao wangepita katika eneo hilo. Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kaseme, Mhe. Andrea Karamla, amewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu na kuepuka vitendo vinavyoweza kuvuruga amani wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.

About