@jukwaahuru: MCHANGE AGOMA KUOMBA RADHI, AWANG'ANG'ANIA HECHE, NILESH NA MPINA Tukutane Mahakamani hata kesho, ndivyo alivyojibu Habibu Mchange Mkurugenzi wa Jamvi media Group akigoma kuomba radhi kutokana na tuhuma alizozitoa kwa Mfanyabiashara Nilesh Suchack kuwa anawatumia wanasiasa wa upinzani John Heche wa CHADEMA na Luhaga Mpina wa ACT Wazalendo kwa ajili ya kufanya upotoshaji katika uagizaji wa mafuta nchini Mchange amesema ataitumia kesi hiyo kuufumbua macho umma wa watanzania juu ya michezo michafu inayofanywa na wafanyabiashara aina ya Nilesh akisema kuwa siku 14 alizopewa ni nyingi sana anamtaka aende mahakamani hata kesho. Ikumbukwe kuwa siku kadhaa zilizopita Nilesh alimuandikia barua Mchange ya kumtaka aombe radhi na kufuta kauli zake ndani ya siku 14 la sivyo atamburuza mahakamani na kumdai fidia ya Tsh Bilioni 12